internet advertising March 18 2017 Elimu inahitajika zaidi ili kukuza sekta ya utalii | DotFIVE

March 18 2017 Elimu inahitajika zaidi ili kukuza sekta ya utalii

   Godwell ole meing`ataki mratibu spanist
Na;Amiri kilagalila
Wamiliki, watendaji na watoa huduma katika shughuli za utalii mkoani Njombe hususani hoteli wameahidi kuongeza juhudi za utendaji kazi licha ya kuwepo kwa changamoto mbali mbali  ili kukuza sekta ya utaliii katika mikoa ya nyanda za juu kusini.
 baadhi ya wamiliki wa hoteli mkoani Njombe wametoa kauli hiyo katika semina ya siku tatu ya mafunzo yenye lengo la kukuza uchumi katika wizara ya mambo ya ndani yanayotekelezwa na mradi wa SPANIST na kufanyika katika ukumbi wa halmashauri  ya wilaya ya Njombe.

Mkurugenzi msaidizi wa mafunzo ya utafiti na takwimu idara ya utalii wizara ya mali asili na utalii PASKASI MWIRY, amesema kuwa kwa sasa sekta ya utalii imekuwa ikifanya kazi kwa kiwango cha chini kutokana na baadhi ya wamiliki wa hoteli kuwa na watumishi wasiokuwa na vigezo sawia katika ufanyaji kazi.

Naye mratibu wa SPANIST mikoa ya Nyanda za juu kusini GODWELL OLE MEING’ATAKI, amesema kuwa lengo la kuendesha mafunzo hayo ni ktoa elimu kwa utoa huduma kutokana na kuwepo kwa rasimali nyingi za asili katika mikoa ya kusini.

Aidha kwa upande wake kaimu katibu tawala uchumi na uzalishaji mkoa wa Njombe LUSUNGU MBEDE amesema kuwa yapo malalamiko mengi katika eneo la utalii kwa wafanyabiashara hususani mlundikano wa kodi na kuahidi, kuwa serikali ya mkoa wa Njombe mpaka sasa inalifanyia kazi suala hilo ili kufanya marekebisho katika baadhi ya sehemu zinazolalamikiwa.


Share on Google Plus

About Amiri kilagalila

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment

0 comments:

Post a Comment